Showing posts with label TEKNOLOJIA. Show all posts
Showing posts with label TEKNOLOJIA. Show all posts

Thursday, June 28, 2007

FRIJI ISIYOTUMIA UMEME

Hii ni habari njema.Habari hii nimeipata kutoka idhaa ya kiswahili BBC.Ni teknolojia itakayotuwezesha kutumia vyombo vya kupoozea kama vile friji bila ya kutumia umeme.Kilichonivutia zaidi, teknolojia hii ilikuwa ikiongelewa na mtanzania mwenzetu aliyefanya utafiti wake nchini Uingereza.Mwandishi wa habari wa BBC alipomuuliza mhandisi huyu,tarehe 13th March 2007, kuwa kwa nini akiwa kama mwafrika asiisaidie nchi yake kuileta teknolojia hii.

Anamjibu,

“Endapo viongozi wetu na watunga sera watataka kupata utaalamu wangu ili uinufaishe nchi yetu niko tayari”

Swali ninalojiuliza ni kwamba, ni kwa nini hawa tuliowapa dhmana ya kutuongoza hawana mikakati madhubuti na endelevu ya kuwatumia wataalamu wetu walioko ughaibuni hata waliopo nyumbani kwa manufa ya nchi yetu?

Je ni ubutu wa fikra?

Je ni kutokujua?

Au ni nini hasa?

Kuongoza ni kuonyesha njia. Kila mmoja atimize wajibu wake