Tuesday, December 2, 2008

TUWAKATAE VIONGOZI WACHAFU,WALAFI NA MAFISADI!!

Hakuna lisilowezekana katika sayari hii izungukayo!Kila jambo lina wakati wake, wakati hubadilika, binadamu hana budi kwenda na mabadiliko hayo vinginevyo atabaki nyuma na kuachwa na wakati.Kwa muda mrefu Afrika imefanywa kuwa nyuma kutokana na uongozi mbaya wa viongozi walafi wapenda madaraka, wenye utajiri wasioweza kuutolea maelezo, walioupata kutoka kwa kidogo kilichopaswa kuwafikia wananchi wao.

Kile kidogo ambacho kingeweza kuinua maisha ya wananchi wao wamekibinafsisha, ni mithili mfugaji mwenye kutamani kupata ongezeko la maziwa kwa ng'ombe wake bila ya kumuongezea lishe,kumtafutia majani mabichi, wametamani kukamua ng'ombe maziwa yote hata waone matone ya damu, na wametamani maziwa hata kwa ng'ombe dume!!!!

Afrika ambayo imepigania uhuru wake kuanzia miaka ya hamsini bado haijawa huru kiuchumi hata kifikra!!, wako wapi mashujaa wetu wa leo?

Wako wapi kina Julius Nyrere, Kwame Nkrumah, Samora Machel, Nelson Mandela wa leo?, ni lini walikoma kuzaliwa ndani ya Afrika viongozi mithili ya hao?, Bado tunashuhudia Afrika ikiliwa kwa nje na nchi tajiri na kwa ndani na viongozi walafi, hali ikiwepo kasi ndogo na sheria iliyolegezwa na nguvu ya pesa kuwazuia wailao kwa ndani pamoja na kukosa ujasiri wa kupambana na wale wailao kwa nje.

Mwalimu Nyerere wakati akizitetea nchi za dunia ya tatu, alipata kuwakemea mabepari, nchi tajiri,walipokuwa wakishinikiza tuwalipe madeni yao, hela waliiyotunyonya na kutukopesha, akawaambia ni sawa na kumtoa damu mgonjwa mahututi,Afrika iko mahututi kichumi bado!!, wazungu wale walimuelewa Mwalimu!!, Ni nani anayeendeleza mapambano hayo kwa kasi ile ile leo?

Leo tunaona jinsi siasa inavyokimbiliwa hata na wanataaluma, wanajua ni rahisi kuneemeka ukiwa huko,hasa kwa walio na dhamiri zilizokufa,wanaothubutu hata kuchota mapesa ya kununua madawa na kununua magari ya kifahari!!, wanasayansi wamekimbilia siasa, kwa staili hii maendeleo yakujaje?

Kuna ujasiri mwingi na thubutu kubwa ambayo viongozi wetu walio safi wanapaswa kutuonyesha, na wasipofanya hivyo, basi umma utawalazimisha kwani wakati wa mabadiliko ukifika hakuna awezaye kuuzuia, na atakayejaribu kufanya hivyo atakuwa anapambana na nguvu kubwa asiyoiweza!!

Hapa Tanzania tumeshuhudia mawaziri wawili Basil Mramba na Daniel Yona wakipandishwa kizimbani kujibu mashitaka ya jinsi walivyotuibia, tunahitaji mwendelezo wa mapambano haya dhidi ya wale wailao nchi nyetu kwa ndani kwani ni wengi na wasiopaswa kuongoza kwa wakati wa sasa!!

Tuwakatae kama Mwalimu alivyotuasa!!!

Tuko kwenye zama nyingine kabisa,, hakuna lisilowezeakana!!!!!

Wednesday, November 5, 2008

CONGRATS OBAMA!

OBAMA, the first black US President, Conratulations to Americans to go beyond racism.

Sunday, October 26, 2008

MOGAE OYEEEEEEEEEEEEEE!

Heko Mogae, Rais mstaafu wa Botswana kwa tuzo ya Mo Ibrahim.Mogae ndiye mshindi wa mwaka 2007 na amejinyakulia kitita cha dola milioni 5 ikiwa ni pamoja na dola laki 2 kila mwaka hadi atakapoondoka duniani.

Ndio, malipo ni hapahapa duniani, alitenda mema kwa watu wake na amelipwa mema kwa aliyotenda!

Laana nayo ni hapahapa duniani, tazama jinsi viongozi wetu matapeli, walafi, walevi wa madaraka, mafisadi na kila aina ya uchafu waondokapo madarakani, ni aibu tu inayobakia kwao kiasi cha kukosa ujasiri tena wa kuishauri jamii waliyokuwa wakiiongoza!

Mogae alipambana na rushwa akapata mafanikio, alipambana na ukimwi akapata mafanikio.Huyu ni Festus Mogae wa Botswana aliyewabwaga wenzake kina Benjamin Mkapa wa Tanzania,Olusagan Obasanjo wa Nigeria na Ahmad Tejan Kabbah wa Siera Leone.

Mwaka 2007 mshindi alikuwa ni Joachim Chisano wa Msumbiji, mwaka 2008 amekuwa ni Festus Mogae. Je miaka michache ijayo baada ya raisi wetu kuachia kiti kuna matumaini yoyote ya kuibuka kidedea?
Kama Mogae na Chisano wameweza kupambana na matatizo ya kisiasa, kijamii na kiuchumi na kupata mafanikio, Kikwete anashindwa nini?

Ingawa yawezekana ikawa muhimu si zile fedha wanazopata bali kutambulika kwa yale mema waliyoyafanya na kubakia kuwa viongozi wa kuigwa!

Yapo matatizo mengi yatuzungukayo!, rushwa,mikataba ya kifisadi,wizi wa EPA, ukimwi, ujinga, umaskini, gharama kubwa za uchangiaji elimu ya juu na mengine kibao!

Kadri miaka ya utawala wa awamu ya nne inavyoondoka tunataka kuona mabo hayo yakipungua kabisa kama si kwisha.Kinachotakiwa ni kuthubutu na kudhamiria kwa ujasiri mkubwa.

Inawezekana!

Huu ni ujumbe wangu kwako Mr President!

Sunday, March 23, 2008

HERI YA PASAKA!

Leo tunaazimisha kufufuka kwa Bwana Yesu miaka 2000 iliyopita,jambo la kujiuliza ni kwamba, kufa na kufufuka kwake Bwana Yesu kumeleta nini katika maisha yetu?, kumeyabadilisha vipi maisha yetu?
Tutafakari.
Baada ya kutafakari na kujibu maswali hayo tusherekee kwa matokeo ya siku hii ya kusherekea kufufuka kwa Bwana Yesu.
Kufufuka kwake kulileta ukombozi wa miili na roho zetu!
Ni siku ya kumshukuru Mungu kwa hilo na kuyapa kisogo mambo yaliyo maovu!
HERI YA PASAKA!!!

Sunday, February 10, 2008

TANZAINIA BILA UFISADI INAWEZEKANA!

Nimeisikiliza ripoti ya kamati teule ya bunge iliyochunguza kampuni iliyopewa zabuni ya kuzalisha umeme, Richmond. Mwenyekiti Mwakyembe katuambia haikuwa na uwezo hata wa kuchomeaka taa kwenye kishikio (bulb holder) chake. Huu ni mzaha mkubwa kwa watanzania, wakuu wale waliopitisha kwa kulazimisha mkataba ule, ripoti ilielezea kama ni watu wenye ujasiri wa kifisadi.Hakika ndivyo walivyo.
Ni kashfa kubwa ambayo Lowasa kwa nguvu ya madaraka yake alishindwa kuizima, kwani kamati iliyoshughulikia swala hilo ilikuwa makini kweli kweli.
Kama ambavyo bunge limeomba mikataba yote sasa iende bungeni ijadiliwe, wahusika si tu, wawajibishwe bali wafilisiwe na washitakiwe!
Ikiwa jamii huapata hasira kwa wezi na vibaka waibao kuku mitaani au kuchoa simu mifukoni kiasisi hata cha kuwachoma moto iweje hasira hiyo ishindwe kuwawakia mafisadi hawa wanaoiba mabilioni yetu?, Moto unaowastahili hawa si wa kiberiti ni maisha ya jela kwani waikosea jamii na wamezidi kuifukarisha jamii yetu na kurudisha nyuma mapambano dhidi ya umasikini!
Tunahitaji kina Mwakyembe kumu tu kuibadili nchi hii ambayo tayari ilishaanza kuoza na kunuka kwa ufisadi.
ALUTA KONTINUA!

Friday, January 4, 2008

IS IT DEMO-CRACY OR DEMO-CRAZY?



Another shame in Africa!!!
As an East African, i am deeply sympathetic of what is going on in Kenya!!, aah!,what is wrong with Africa?. Every one could see that something was wrong in the whole process of counting the votes!,only re election will clear the doubt,in this Kibaki has no choice, re counting may not give something different, anyway let the Kenyans decide!, we don't want to see more blood of our fellow Africans.
We want peace in Kenya.
We want peace in East Africa.
We want peace in Africa!