Sunday, October 26, 2008

MOGAE OYEEEEEEEEEEEEEE!

Heko Mogae, Rais mstaafu wa Botswana kwa tuzo ya Mo Ibrahim.Mogae ndiye mshindi wa mwaka 2007 na amejinyakulia kitita cha dola milioni 5 ikiwa ni pamoja na dola laki 2 kila mwaka hadi atakapoondoka duniani.

Ndio, malipo ni hapahapa duniani, alitenda mema kwa watu wake na amelipwa mema kwa aliyotenda!

Laana nayo ni hapahapa duniani, tazama jinsi viongozi wetu matapeli, walafi, walevi wa madaraka, mafisadi na kila aina ya uchafu waondokapo madarakani, ni aibu tu inayobakia kwao kiasi cha kukosa ujasiri tena wa kuishauri jamii waliyokuwa wakiiongoza!

Mogae alipambana na rushwa akapata mafanikio, alipambana na ukimwi akapata mafanikio.Huyu ni Festus Mogae wa Botswana aliyewabwaga wenzake kina Benjamin Mkapa wa Tanzania,Olusagan Obasanjo wa Nigeria na Ahmad Tejan Kabbah wa Siera Leone.

Mwaka 2007 mshindi alikuwa ni Joachim Chisano wa Msumbiji, mwaka 2008 amekuwa ni Festus Mogae. Je miaka michache ijayo baada ya raisi wetu kuachia kiti kuna matumaini yoyote ya kuibuka kidedea?
Kama Mogae na Chisano wameweza kupambana na matatizo ya kisiasa, kijamii na kiuchumi na kupata mafanikio, Kikwete anashindwa nini?

Ingawa yawezekana ikawa muhimu si zile fedha wanazopata bali kutambulika kwa yale mema waliyoyafanya na kubakia kuwa viongozi wa kuigwa!

Yapo matatizo mengi yatuzungukayo!, rushwa,mikataba ya kifisadi,wizi wa EPA, ukimwi, ujinga, umaskini, gharama kubwa za uchangiaji elimu ya juu na mengine kibao!

Kadri miaka ya utawala wa awamu ya nne inavyoondoka tunataka kuona mabo hayo yakipungua kabisa kama si kwisha.Kinachotakiwa ni kuthubutu na kudhamiria kwa ujasiri mkubwa.

Inawezekana!

Huu ni ujumbe wangu kwako Mr President!