Sunday, February 10, 2008

TANZAINIA BILA UFISADI INAWEZEKANA!

Nimeisikiliza ripoti ya kamati teule ya bunge iliyochunguza kampuni iliyopewa zabuni ya kuzalisha umeme, Richmond. Mwenyekiti Mwakyembe katuambia haikuwa na uwezo hata wa kuchomeaka taa kwenye kishikio (bulb holder) chake. Huu ni mzaha mkubwa kwa watanzania, wakuu wale waliopitisha kwa kulazimisha mkataba ule, ripoti ilielezea kama ni watu wenye ujasiri wa kifisadi.Hakika ndivyo walivyo.
Ni kashfa kubwa ambayo Lowasa kwa nguvu ya madaraka yake alishindwa kuizima, kwani kamati iliyoshughulikia swala hilo ilikuwa makini kweli kweli.
Kama ambavyo bunge limeomba mikataba yote sasa iende bungeni ijadiliwe, wahusika si tu, wawajibishwe bali wafilisiwe na washitakiwe!
Ikiwa jamii huapata hasira kwa wezi na vibaka waibao kuku mitaani au kuchoa simu mifukoni kiasisi hata cha kuwachoma moto iweje hasira hiyo ishindwe kuwawakia mafisadi hawa wanaoiba mabilioni yetu?, Moto unaowastahili hawa si wa kiberiti ni maisha ya jela kwani waikosea jamii na wamezidi kuifukarisha jamii yetu na kurudisha nyuma mapambano dhidi ya umasikini!
Tunahitaji kina Mwakyembe kumu tu kuibadili nchi hii ambayo tayari ilishaanza kuoza na kunuka kwa ufisadi.
ALUTA KONTINUA!