Monday, July 9, 2007

Kauli ya Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa,Ban Ki-Moon

“Mazoea yangu kila siku asubuhi huenda hayatofautiani na yako. Tunachukua magazeti na kufungua television,iwe mjini New York,Lagos au Jakarta kuangalia mateso ya kila siku yanayomkabili binadamu.Inawezekana kuwaDarfur,Lebanon au Somalia”

Anaendelea …………………………. na kumalizia,

“Kila asubuhi tunaweza kusoma kwenye magazeti. Lakini ni kwa jinsi gani tunasikiliza sauti za watu hao au kujaribu kwa nguvu zote na kwa kudhamiria kuwasaidia?Nawaomba mfanye hivyo”

Hii ni kauli nzito inayotoka kwenye hisia kali za kiongozi anayewajali watu anayewaelekeza viongozi kuwa watumishi wa watu.Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-Moon anachojaribu kuwaeleza viongozi hawa ni kuwa haya mateso tunayoyaona kwenye runinga, tunayoyasoma kwenye magazeti na tunayoyasikia kwenye radio wasiyapuuze, wasiyaangalie tu, wasiyasome tu.Wayatatue kwa nguvu zao zote.

Ni kama vile anawaambia huu ni wajibu wenu muutekeleze.

Ni kama vile anawaambia mshikwe na huruma mnapoona na kusoma matatizo yanayowazunguka watu wenu na kuutafuta ufumbuzi wa matatizo hayo.

Ni kama vile anawaambia msiidharau sauti ya watu inapobeba kero zao na kuzileta kwenu, zitatueni kero zao.

Ni viongozi wanagpi tulionao hapa Tanzania wanaolitekeleza ombi hilo la Katibu mkuu kwa vitendo?,Wananchi wengi ukiwsaikiliza wamechoka, wamepoteza matumaini kwa viongozi waliowachagua. Hakuna anayemjali mskini.Koti la umaskini wa watu wamelitupa, watalivaa tena wakati wauchaguzi ukiwadia. Ndio nchi hii ilipofikia.Watanganyika sasa wanaitwa Wadanganyika!.Tunadanganywa na viongozi miaka mitano mitano!

Hivi yale maisha bora kwa kila mtanzania tuliyoambiwa yako wapi?

Kwa mujibu wa nukuu ya Ban Ki-Moon hapo juu, ni kiongozi gani, ni mbunge gani anayeweza kunyoosha kidole akasimama akatueleza namna anavyotumia mudawake kutatua kero za watu anaowaongoza?. Unatoka wapi uhalali wa viongozi butu kama hawa kuendelea kuongoza?. Mbona hawazisikii sauti za watu na kuwasaidia?

Wa kale walisema “sauti ya watu ni sauti ya Mungu”,mbona wameikana busara hii ya wazee wetu wa zamani?

Kuna ufisadi mwingi unaotuzunguka, kuuacha upite nakuendelea kwenye kizazi kijacho ni kutokitendea haki kizazi hicho cha wana wetu na wana wa wana wetu.Ni kutokuwajibika.Iwe kwa mijadala au njia yoyote ile tunahitaji mabadiliko!Mbona tuliupigania uhuru, lakini matunda yake tumeyaacha yawafaidishe wajanja wachache?Hakika kizazi hiki kina jukumu kubwa la kufanya kuuondoa uozo uliopo.Mafisadi hawa wameingia mikataba mibovu kwa maslahi yao. Bado wengine wangali wakikalia viti vyao.Kwa nini?

Yule mkuu wa Benki ya dunia alipopata kashfa ya kumpandisha cheo mpenzi wake na kumuongezea mshahara,sasa amewekwa pembeni.Mbona hapa kwetu huyu mkuu wa benki kuu ana tuhuma za ulaji anaendelea kukalia kiti? Si inasemekana anatarajiwa kuchunguzwa?.Taifa hili linahitaji muelekeo mpya. Linahitaji kuwa na utaratibu wa kuwatambua wenye maadili wanaofaa kuongoza lakini pia kuwe na utarataratibu wa kuwachukulia hatua kali wanaokwenda kinyume na taratibu hizo bila kulindana.

Viongozi wetu watekeleze wito wa katibu mkuu, Ban Ki-Moon.

Mungu ibariki Tanzania,

Mungu ibariki Afrika.

No comments: