Sunday, October 21, 2007

WATU WAOVU WAMEMUUA LUCKY DUBE!

Ni mchana wa ijumaa niko sehemu napata msosi wa mchana, pembeni jamaa anaongea na mwenzake, Lucky Dube amefariki, nayasikia maongezi yale, kwa kuwa sikuwa mbali na meza yao.Nashangaa!.Namuuliza mmoja wao , ananiambia ni kweli jamaa wamemuua Lucky Dube.Jioni siku hiyo hiyo ya ijumaa nasikiliza Voice of America, nasikia wanatangaza kuwa Lucky Dube ameuwawa.

Nikiwa njiani nakutana na ajali daladala,DCM, imeuvaa mti, mtu mmoja amefariki, mwili wake ukiwa bado umelala barabarani!
Maisha ni safari yenye mwisho,hakuna ajuaye mwisho huu unafika lini!,Lucky Dube hakujua kama siku ile angeaga dunia,watu wasio na utu wamemuua, ni watu wenye dhamiri zilizokufa tu, ndio wawezao kufanya kitendo cha kinyama kiasi hicho!

Kijana yule angejua kuwa gari lile lingepata ajali asingalipanda daladala lile!,kifo ni kitu ambacho tumefichwa tusijue kinakuja lini na kwa staili gani!
Anyaway, maisha hayana budi kuendelea!

Ni aina ya uaimbaji wake na ujumbe ndani nyibo zake ndizo zinisukumazo kuandika juu yake.South Afrika na Afrika kwa ujumla imempoteza
mpambanaji dhidi ya ubaguzi wa rangi,mwanamapinduzi na mpigania haki za watu wanyonge Lucky Dube!

He has gone but the messages in his songs will continue to live!

No comments: